Swahili News
- UAE: Iran imeshambulia meli katika Mlango-Bahari wa Hormuz July 14, 2026Umoja wa Falme za Kiarabu UAE, umesema leo kuwa meli zake mbili za mafuta za taifa hilo zililengwa na makombora mawili ya masafa marefu ya Iran katika njia ya kusini ya Mlango-Bahari wa Hormuz.
- Kesi dhidi ya Besigye yaanza bila kuwepo mawakili wake July 14, 2026Kesi ya uhaini inayomkabili kiongozi wa upinzani nchini Uganda, Dkt. Kizza Besigye, ilianza kusikilizwa jana katika mahakama kuu ya Uganda, lakini bila ya kuwepo kwa mawakili wake wakuu.
- Kallas: Kuna uwezekano wa vikwazo dhidi ya Israel July 14, 2026Mkuu wa sera za mambo ya nje wa Umoja wa Ulaya Kaja Kallas, amesema kuna uwezekano wa kufikiwa kwa makubaliano ya kuweka vikwazo kwenye biashara ya bidhaa zinazotoka katika makazi ya walowezi wa Israel.
- Zaidi ya wahamiaji 53,000 waondoka Afrika Kusini July 14, 2026Afrika Kusini imewafukuza au kuwarejesha makwao kwa hiari zaidi ya wahamiaji 53,000 wa Kiafrika ndani ya kipindi cha mwezi mmoja, katika operesheni ya mamlaka inayolenga kudhibiti uhamiaji haramu.
- Urusi yafanya mashambulizi mapya ya makombora dhidi ya Kiev July 14, 2026Urusi imefanya mashambulizi mapya ya usiku kucha ya makombora ya balistiki dhidi ya mji mkuu wa Ukraine Kiev huku milipuko kadhaa ikisikika katikati ya jiji. Haya yamesemwa leo na mamlaka nchini Ukraine.
- Marekani yafanya mashambulizi mapya dhidi ya Iran July 14, 2026Marekani imefanya mashambulizi mapya dhidi ya Iran mapema leo, ikiwa ni hatua mpya ya kuongezeka kwa mapigano, licha ya Rais wa Marekani, Donald Trump, kusema kuwa makubaliano na Tehran bado yanawezekana.
- Kesi ya Besigye yaunguruma bila mawakili kuhudhuria mahakamani July 13, 2026Kesi ya uhaini dhidi ya kiongozi wa upinzani nchini Uganda, Kizza Besigye, imeanza Jumatatu bila mawakili wa utetezi, baada ya mmoja wao kutiwa gerezani na mwingine kuzuiwa kuingia nchini nchini humo na mamlaka.
- Iran na Marekani zinadai kuidhibiti Hormuz July 13, 2026Marekani na Iran zimeendelea kutangaza kila mmoja kuudhibiti Mlango Bahari wa Hormuz, baada ya kushambuliana mwanzoni mwa wiki katika maeneo tofauti ya Mashariki ya kati.
- Trump arejesha mzingiro wa Hormuz, atangaza tozo kwa meli July 13, 2026Trump amesema Marekani inarejesha mzingiro dhidi ya Iran katika Mlango-Bahari wa Hormuz na itatoza meli ada kwa kupita salama. Iran imekataa hatua hiyo huku mvutano ukiongeza hofu kwa biashara na soko la mafuta duniani.
- China yatuma ujumbe mpya wa nguvu za nyuklia July 13, 2026China imefanya jaribio lake kubwa zaidi la kombora la masafa marefu tangu mwaka 2024, kwa kulirusha kutoka manowari ya nyuklia kuelekea kusini mwa Bahari ya Pasifiki. Beijing imesema ni zoezi la kawaida la kijeshi.
- Maisha chini ya utawala wa makundi ya kigaidi Sahel July 13, 2026Ukanda wa Sahel barani Afrika umegeuka kuwa kitovu kikuu cha ugaidi duniani, huku makundi yenye itikadi kali yakipanua shughuli zake kutoka maeneo ya vijijini hadi miji mikubwa, na kuzusha na machafuko katika eneo hilo.
- Utafiti: Wanasiasa Kenya waajiri makundi ya vurugu kuelekea uchaguzi wa 2027 July 13, 2026Ripoti mpya nchini Kenya inaonya kuwa kuongezeka kwa matumizi ya vijana wanaolipwa kuvuruga mikutano ya kisiasa na maandamano yanaongezeka, jambo linaloweza kuchochea ghasia kuelekea uchaguzi mkuu wa 2027.
- Aliyekuwa Emir wa Qatar Sheikh Hamad afariki akiwa na miaka 74 July 13, 2026Aliyekuwa Emir wa Qatar Sheikh Hamad bin Khalifa Al Thani, aliyeibadilisha Qatar kutoka taifa dogo la Ghuba kuwa kitovu cha diplomasia, biashara, vyombo vya habari na michezo duniani, amefariki dunia kwa umri wa miaka 74
- Kongo: Jeshi lapiga marufuku matumizi ya simu janja vitani July 13, 2026Jeshi la Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo limewapiga marufuku wanajeshi kutumia simu janja bila idhini vitani, likisema hatua hiyo imehatarisha usalama wa taifa na kuchangia kushindwa kwa baadhi ya operesheni za kijeshi.
- Jenerali mwenye msimamo mkali wa Iran aibuka mhusika muhimu July 13, 2026Wakati mazungumzo kati ya Iran na Marekani kuhusu uwezekano wa kumaliza vita yakiendelea katika hali ya sintofahamu, jina la Brigedia Jenerali Ahmad Vahidi limeibuka tena katikati ya maamuzi muhimu ya kisiasa na kijeshi.
