Swahili News
- Zelenskiy amwondoa balozi wa Ukraine nchini Marekani August 4, 2026Rais Volodymyr Zelenskiy amemwondoa Olha Stefanishyna katika wadhifa wa balozi wa Ukraine nchini Marekani, wakati Kyiv ikibadilisha viongozi wakuu na kutafuta silaha zaidi kutoka Washington.
- Ugonjwa wa Ebola wawaua watu 1700 mashariki mwa Kongo August 4, 2026Ugonjwa wa Ebola umeua zaidi ya watu 1,700 mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo. Haya ni kwa mujibu wa takwimu za serikali ya nchi hiyo.
- Shambulizi la droni la nchini Sudan lawaua watu 35 August 4, 2026Takriban watu 35 wameuawa baada ya shambulio la droni linalodaiwa kufanywa na jeshi la Sudan kulenga jengo la mahakama ya kiraia katika eneo la Darfur.
- Marekani ina matumaini ya kufunguliwa kwa Hormuz August 4, 2026Marekani imesema ina matumaini kuwa makubaliano ya kufungua tena Mlango-Bahari wa Hormuz yatafikiwa leo au kesho. Haya ni kulingana na waziri wa fedha wa nchi hiyo, Scott Bessent.
- Uhispania: Mkutano wa Ulaya juu ya Ceuta ulikuwa wa tija August 4, 2026Mkutano wa mawaziri wa mambo ya ndani wa Umoja wa Ulaya kuhusu wimbi kubwa la wahamiaji waliovuuka mpaka wa Morocco na kuingia jimbo linalomilikiwa na Uhispania kaskazini mwa Afrika, Ceuta, ulifanyika kwa mafanikio.
- Maghala ya kampuni ya Wildberries yashambuliwa nchini Urusi August 4, 2026Mashambulizi ya usiku kucha ya droni za Ukraine yamelenga maghala matatu ya kampuni kubwa ya biashara ya mtandaoni ya Wildberries nchini Urusi na kusababisha vifo vya watu watano.
- Hamas yakubali kuondoa silaha, lakini mpango utafanikiwa? August 4, 2026Hamas imekubali mpango wa kuondoa silaha na kukabidhi utawala wa Gaza kwa kamati ya Wapalestina. Lakini Israel haijatoa jibu rasmi, huku maswali mazito yakibaki kuhusu utekelezaji na usimamizi wake.
- Israel yajenga ukuta unaogawanya Gaza: Hatua ya usalama au mpaka mpya? August 4, 2026Israel imeanza kujenga ukuta mrefu wa udongo ndani ya Ukanda wa Gaza katika eneo linalodhibitiwa na jeshi lake, ikisema hatua hiyo inalenga kuimarisha usalama. Lakini Wapalestina wanahofia mgawanyiko wa kudumu.
- Mashambulizi Gaza yatia mashakani mpango wa Trump August 4, 2026Wapalestina wanasema mashambulizi mapya ya Israel na kupanuka kwa maeneo yanayodhibitiwa na jeshi lake vinapunguza matumaini ya kutekelezwa kwa mpango wa Trump wa kumaliza vita Gaza.
- Wadudu wadogo, hasara kubwa: Biashara ya siafu yashamiri August 4, 2026Biashara halali na haramu ya siafu kutoka Afrika kwenda Ulaya inashamiri. Wafugaji wanavutiwa na wadudu hao, lakini wataalamu wanaonya kuhusu ujangili na hatari kubwa kwa mifumo ya ikolojia.
- Byanyima amtaka Museveni amwachie Besigye kwa sababu za kiafya August 4, 2026Winnie Byanyima amemtaka Rais Yoweri Museveni amwachie Dkt. Kizza Besigye, akisema hali yake ni mbaya baada ya kuanguka mahakamani na kulazwa katika chumba cha wagonjwa mahututi.
- Azimio wajipanga upya kuelekea uchaguzi wa Kenya wa 2027 August 4, 2026Muungano wa Azimio umefanya mabadiliko ya uongozi na muundo wake, ukimjumuisha Fred Matiang'i katika baraza lake la juu, huku ukijaribu kujiimarisha kuelekea uchaguzi mkuu wa Kenya wa mwaka 2027.
- Meli ya mizigo yaripoti kushambuliwa Hormuz August 4, 2026Shirika la kufuatilia usalama wa shughuli za baharini la Uingereza, UKMTO, limesema meli moja ya mizigo imeshambuliwa kwa kombora lisilojulikana upande wa Oman kwenye Mlango wa Bahari wa Hormuz.
- Besigye ni dhaifu na hawezi kuzungumza, asema mkewe August 4, 2026Kiongozi wa upinzani nchini Uganda, Kizza Besigye, ni dhaifu sana na hawezi kuzungumza wala kuandika, amesema mkewe Winnie Byanyima baada ya kumtembelea katika Hospitali ya Mulago.
- Utafiti waeleza kwa nini vijana wako hatarini zaidi kupata saratani August 4, 2026Watafiti wamegundua ongezeko la baadhi ya aina za saratani zinazohusishwa na umri miongoni mwa vijana. Utafiti mpya unaonyesha huenda sababu ni kwamba vijana wanazeeka kibayolojia kwa kasi zaidi kuliko wazazi wao.
