RSS feed: Swahili News Swahili News

  • Ushirikiano wa BRICS wataka kuimarisha nguvu zaidi dhidi ya magharibi September 14, 2026
    Waziri Mkuu wa India, Narendra Modi ameonya juu ya ongezekao la mvutano wa kisiasa na kimaeneo ulimwenguni, kuvurugika kwa minyororo ya ugavi na mizozo ya hali ya hewa na namna inavyoendelea kuathiri watu kote duniani.
  • Safari ya mgonjwa yazua hofu ya kusambaa kwa Ebola September 13, 2026
    Kisa cha Ebola kimethibitishwa jimboni Sud-Ubangi, mbali na kitovu cha mlipuko mashariki mwa DRC. Mgonjwa aliyefariki alisafiri kupitia Rwanda na Uganda, na kuzua hofu ya kuwapo kwa watu wengi waliokutana naye njiani.
  • Trump azuru Ireleand, apigia chapuo kuungana tena September 13, 2026
    Rais Donald Trump amesema angependa kuona Ireland Kaskazini ikiungana na Jamhuri ya Ireland, kauli iliyoibua mjadala kuhusu suala nyeti la kisiasa na mustakabali wa eneo hilo ambalo kwa sasa ni sehemu ya Uingereza.
  • Usalama waimarishwa Nairobi kuelekea mkutano wa Sifuna September 13, 2026
    Mamlaka za usalama zimeimarisha doria na kuweka maafisa wengi wa polisi katika maeneo muhimu ya Nairobi kufuatia mkutano mkubwa wa kisiasa ulioratibiwa na kiongozi wa upinzani Edwin Sifuna.
  • Mfalme Oyo Nyimba wa Tooro azikwa nchini Uganda September 12, 2026
    Mfalme wa Tooro nchini Uganda, Oyo Nyimba Kabamba Iguru Rukidi wa Nne, aliyewahi kutambulika kama mfalme mdogo zaidi duniani, amezikwa Jumamosi katika Makaburi ya Kifalme ya Karambi magharibi mwa Uganda.
  • Eritrea yaishutumu Ethiopia kwa "kuvuruga uthabiti" wa Pembe ya Afrika September 12, 2026
    Serikali ya Eritrea imemshutumu jirani yake "kuvuruga uthabiti wa eneo la Pembe ya Afrika", wakati mvutano kati ya mataifa hayo mawili ukiendelea kuongezeka na kuzua hofu ya kuzuka kwa mzozo mpya wa kijeshi.
  • Zelensky aonyesha utayari wa kukutana na Putin katika mkutano wa G20 mjini Miami September 12, 2026
    Katika mahojiano na DW, Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky amesema yuko tayari kukutana ana kwa ana na mwenzake wa Urusi Vladimir Putin katika mkutano wa G20 unaotarajiwa kufanyika Miami nchini Marekani Desemba, 2026.
  • Viongozi mbalimbali wawasili India kwa mkutano wa BRICS September 11, 2026
    Viongozi mbalimbali wa dunia wamewasili mjini New Delhi, India, kwa mkutano wa BRICS unaotarajiwa kuanza rasmi kesho, Jumamosi. Baadhi ya viongozi hao tayari wameanza mikutano ya awali na mazungumzo ya pande mbili.
  • 9/11: Nadharia za njama zinazoendelea kusambaa September 11, 2026
    Miaka 25 baada ya mashambulizi ya Septemba 11, nadharia mbalimbali za njama bado zinasambaa. Ni madai gani yanayotolewa, ukweli unasemaje na kwa nini baadhi ya watu wanaendelea kuyaamini?
  • Kwa nini watu bado huamini 9/11 ilikuwa njama ya ndani? September 11, 2026
    Mwaka 2023, Mmarekani mmoja kati ya watano bado aliamini serikali ilihusika katika mashambulizi ya 9/11. Kwa nini nadharia hiyo inaendelea kusambaa licha ya ushahidi unaoikanusha?
  • Miaka 25 baada ya 9/11: Al-Qaeda imekuwaje? September 11, 2026
    Miaka 25 baada ya mashambulizi ya 9/11, Al-Qaeda si tena mtandao wa kigaidi wa kimataifa uliokuwa zamani. Uongozi wake umedhoofika, lakini matawi yake Afrika na Asia yanaendelea kuimarika kupitia migogoro ya ndani.
  • Twin Towers: Kutoka mwaka 1946 hadi Ground Zero September 11, 2026
    Kwa karibu miaka 30, majengo ya Twin Towers yalikuwa alama ya jiji la New York na nguvu ya uchumi wa Marekani. yalijengwa kama kitovu cha biashara ya dunia, lakini yakawa shabaha ya mashambulizi ya Septemba 11, 2001.