Swahili News
- Trump alakiwa kwa mapokezi ya heshima na jeshi la China wakati alipowasili Beijing May 13, 2026Rais wa Marekani Donald Trump amewasili Beijing kwa mkutano muhimu wa ngazi ya juu na kiongozi wa China Xi Jinping, mkutano unaolenga kupunguza mvutano kati ya mataifa hayo mawili yenye nguvu duniani.
- Mfalme Charles afungua bunge / Starmer aandamwa kisiasa May 13, 2026Nchini Uingereza, Mfalme Charles wa Tatu amefungua rasmi kikao kipya cha Bunge kwa hotuba iliyoweka wazi ajenda ya serikali kwa mwaka ujao. Hayo yanafanyika wakati Keir Starmer akikabiliwa na mgogoro mkubwa wa kisiasa.
- Rais Donald trump awasili Beijing kwa mazungumzo na Xi Jinping May 13, 2026Rais wa Marekani Donald Trump amewasili Beijing kwa mazungumzo yanayosubiriwa kwa hamu na Rais Xi Jinping wa China yatakayojikita katika mzozo wa nchini Iran, biashara na uamuzi wa Marekani kuiuzia silaha Taiwan.
- Urusi yarejelea "masharti magumu" ili kuvimaliza vita vya Ukraine May 13, 2026Urusi imerudia tena hii leo masharti yake magumu ya kukomesha vita vya Ukraine, na kuondoa uwezekano wa kusitisha mapigano au mazungumzo ya kina na Ukraine hadi pale itakapojiondoa kwenye mkoa wa mashariki wa Donbas.
- WFP yapunguza msaada wa chakula, Syria May 13, 2026Umoja wa Mataifa umesema leo kwamba unapunguza msaada wa dharura wa chakula kwa Syria kwa asilimia 50 na kusitisha mpango wa ruzuku ya mkate ambao umesaidia mamilioni ya watu, kutokana na uhaba wa fedha.
- Uturuki na Armenia warejesha uhusiano wa kibiashara May 13, 2026Uturuki imeondoa vizuizi vya moja kwa moja vya kibiashara na Armenia, ikiwa ni ishara ya kuimarika kwa uhusiano kati ya maadui hao wa muda mrefu.
- UN yakemea mashambulizi ya anga kaskazini mwa Nigeria May 13, 2026Umoja wa Mataifa walaani mashambulizi ya anga Nigeria na Chad baada ya takriban raia 100 kuuawa Jumapili, katika tukio kubwa la umwagaji damu kaskazini mwa nchi.
- Urusi na Ukraine waendelea kushambuliana baada ya usitishaji vita wa muda May 13, 2026Mashambulizi mapya ya ndege zisizo na rubani, hatua ya Urusi kujaribu kombora jipya la nyuklia na kauli tata za Moscow kuhusu mwisho wa vita, vinaonyesha kuwa vita kati ya Urusi na Ukraine bado viko mbali kumalizika.
- Rais Trump aenda China kusaka fursa zaidi za biashara Rais Trump aenda China, ataka fursa zaidi za biashara May 13, 2026Rais Donald Trump amesema atamuomba Rais wa China Xi Jinping kuyafungulia milango zaidi makampuni ya Marekani, wakati akielekea nchini humo kwa mkutano wa kilele unaosubiriwa kwa hamu.
- Starmer aapa kuendeleza ajenda ya mageuzi May 13, 2026Waziri Mkuu wa Uingereza Keir Starmer ameapa kuendelea na ajenda yake ya mageuzi huku akipambana kuokoa nafasi yake madarakani
- Je, kuna uwezekano wa serikali ya muungano Zanzibar? May 13, 2026Baada ya ukimya wa kisiasa, dalili za matumaini zajitokeza Zanzibar. Viongozi wa CCM na ACT wazungumzia uwezekano wa kurudi kwa Serikali ya Umoja.
- Trump aitaka China ifungue milango ya biashara kwa Marekani May 13, 2026Rais wa Marekani Donald Trump amesema atamshinikiza Rais wa China, Xi Jinping "afungue fursa zaidi" kwa kampuni za Marekani kufanya biashara nchini China.
- Hegseth: Jeshi la Marekani linahitaji bajeti ya dola trilioni 1.5 May 13, 2026Waziri wa ulinzi wa Marekani Pete Hegseth ameliambia bunge la seneti nchini humo kuwa utawala wa Rais Trump unahitaji dola trilioni 1.5 kama bajeti ya jeshi la nchi hiyo kwa mwaka 2027.
- Qatar yaionya Iran isitumia Mlango Bahari wa Hormuz kuzishinikiza nchi za Ghuba May 12, 2026Qatar imesema Iran haipaswi kutumia Mlango Bahari wa Hormuz, iliyoufunga tangu kuanza kwa vita vya Marekani na Israel dhidi ya Jamhuri hiyo ya kiislamu Fenruari 28, kama njia ya kuyahadaa mataifa ya Ghuba.
- Ulemavu wa kudumu unaotokana na kuugua Kisukari May 11, 2026Ripoti zinazohusiana na masuala ya afya nchini Tanzania zinaonesha kuongezeka kwa magonjwa yasiyoambukiza hususan ugonjwa wa kisukari.
