Swahili News
- Mfumo wa Pamoja wa Hifadhi wa Umoja wa Ulaya, waleta hofu kwa waomba hifadhi June 3, 2026Wakati EU ikijiandaa kuanza kutekeleza mfumo mpya wa pamoja wa kudhibiti utoaji hifadhi na uhamiaji, wataalamu waonya hatua hizo huenda zikaongeza ugumu kwa watu wanaotafuta hifadhi badala ya kutatua tatizo la msingi.
- Hali ya demokrasia na usalama mashakani Msumbiji June 3, 2026Wimbi la mauaji na mashambulizi dhidi ya wanasiasa wa upinzani nchini Msumbiji limeibua wasiwasi kuhusu hali ya demokrasia na usalama nchini humo.
- Mgomo wa kupinga mabadiliko ya katiba wafanyika Kongo June 3, 2026Wakaazi wengi wa mjini Kinshasa nchini Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo, wameitikia mwito wa upinzani wa kutokwenda kazini kama sehemu ya kupinga kupitishwa kwa muswada wa sheria ya mabadiliko ya katiba.
- Iran yaonya mashambulizi zaidi Marekani ikiendeleza uchokozi June 3, 2026Mshauri wa kijeshi wa kiongozi mkuu wa Iran, Mohsen Rezaei, ameonya leo kuwa kutakuwa na mashambulizi zaidi ya makombora na droni iwapo Marekani itaendeleza mashambulizi yake nchini Iran.
- Mahakama ya Kenya yasimamisha kujengwa kituo cha karantini June 3, 2026Mahakama Kuu ya Kenya Jumanne ilisimamisha kwa wiki tatu zaidi mpango wa kujenga kituo cha karantini ya Ebola, kilichopendekezwa na Marekani .
- Ukraine yashambulia kwa droni mji wa St Petersburg, Urusi June 3, 2026Rais wa Ukraine, Volodymyr Zelensky, amesema vikosi vyake vimeshambulia kwa droni mji wa Saint Petersburg nchini Urusi leo asubuhi, saa chache kabla ya kufunguliwa kwa kongamano la kimataifa la uchumi mjini humo.
- Rais Samia ziarani Urusi June 3, 2026Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan ameanza ziara ya kitaifa ya siku tatu Urusi, ambapo anatarajiwa kukutana na Rais Vladmir Putin katika wakati ambapo sifa ya Tanzania inazidi kuchafuka kwenye nchi za Magharibi.
- UNICEF yaonya kuhusu gharama za kusafirisha misaada June 3, 2026Mkuu wa mipango wa Shirika la Umoja wa Kimataifa la Kuhudumia Watoto, UNICEF, Jean-Cédric Meeùs, amesema jana kuwa mvutano wa Mashariki ya Kati unaongeza gharama za kutoa misaada ya kibinadamu.
- Ujerumani yakabiliwa na ushindani kuwania kiti cha UN June 3, 2026Ujerumani inakabiliwa na ushindani mkubwa katika uchaguzi wa leo ambapo inatafuta kiti cha muda katika Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa, chombo chenye mamlaka makubwa zaidi ndani ya Umoja wa Mataifa.
- Mashambulizi mapya yatikisa Ghuba ya Uajemi June 3, 2026Marekani na Iran zimeendeleza mashambulizi katika Ghuba ya Uajemi na kuzidisha mvutano katika eneo hilo. Mapigano hayo yanatokea wakati juhudi za amani zikiwa bado zimekwama bila mafanikio makubwa.
- Marekani, Iran zashambuliana wakati mazungumzo yakikwama June 3, 2026Jeshi la Marekani limefanya mashambulizi kwenye maeneo mbalimbali ya Iran, huku nayo Iran ikivurumisha makombora na droni kuelekea vituo vya kijeshi na ulinzi vya Marekani kwenye mataifa kadhaa ya Ghuba.
- Urusi yakabiliwa na mashambulizi makali ya droni za Ukraine June 3, 2026Jeshi la Urusi linasema limezidunguwa droni tatu kwenye mkoa wa Leningrad uliopo kaskazini magharibi mwa mji mkuu, Moscow, ikiwa ni muda mchache kabla ya ufunguzi wa jukwaa la kila mwaka la uchumi.
- Mazungumzo ya usitishaji vita kati ya Israel na Lebanon yaanza mjini Washington June 2, 2026Mabalozi wa Israel na Lebanon wameanza duru mpya ya mazungumzo ya moja kwa moja mjini Washington, baada ya Rais wa Marekani Donald Trump kusema alipokea ahadi kutoka pande zote mbili juu ya kupunguza mvutano uliopo.
- Mvutano Israel–Hezbollah waingia hatua mpya June 2, 2026Mvutano kati ya Israel na Hezbollah unazidi kupamba moto huku jitihada za kusaka usitishaji mapigano zikiendelea, Lebanon ikisisitiza kusimamishwa kwa mashambulizi na Marekani ikidai makubaliano ya awali yamefikiwa.
- Kenya haijapiga hatua kwenye vita dhidi ya matumizi ya Sigara June 2, 2026Kenya imesalia nyuma kwenye vita dhidi ya matumizi ya sigara ukilinganisha na mataifa mengine barani Afrika. Ijapokuwa bidhaa za uraibu wa sigara zisizowashwa moto zipo,bei yake iko juu.
