Swahili News
- EU kutoa msaada wa wa euro Milioni 235 kwa Afrika Magharibi na Kati April 23, 2026Umoja wa Ulaya umetangaza kuwa watatoa kiasi cha euro milioni 275 kama msaada wa kiutu kwa ajili ya watu wanaoishi katika maeneo yenye migogoro Afrika Magharibi na Afrika ya Kati.
- Tume ya uchunguzi wa matukio ya uchaguzi wa Oktoba 2025 Tanzania yakabidhi ripoti April 23, 2026Ripoti ya Tume ya uchunguzi wa matukio ya uvunjifu wa amani wakati na baada ya uchaguzi wa Oktoba 29, 2025 nchini Tanzania imewasilishwa Alhamisi, katika mkutano uliohudhuriwa na Rais wa nchi hiyo Samia Suluhu Hassan.
- Awamu ya pili ya mazungumzo ya Israel na Lebanon kufanyika Washington April 23, 2026Wawakilishi wa Israel na Lebanon katika mazungumzo yanayolenga kutafuta amani wanatazamiwa kufanya awamu ya pili ya majadiliano yaliyopangwa kufanyika baadaye Alhamisi mjini Washington nchini Marekani.
- Umoja wa Ulaya wakutana Cyprus kujadili mizozo ya kikanda na bajeti April 23, 2026Viongozi wa Umoja wa Ulaya wanakutana kwenye mazungumzo ya siku mbili yanaolenga kuijadili migogoro inayoyakabili maeneo yanayoizunguka jumuiya yao. Mkutano huo unafanyika katika taifa la Cyprus.
- Uingereza, Ufaransa zaifikia makubaliano ya kudhibiti uhamiaji April 23, 2026Uingereza na Ufaransa zimeafikiana kuhusu mkataba mpya wa miaka mitatu unaolenga kukomesha uhamiaji haramu kwa njia ya mkondo wa bahari uunaopita kati ya mataifa hayo.
- Bomba la Druzhba laanza kutiririsha mafuta kwenda Slovakia April 23, 2026Slovakia imeaanza kupokea mafuta baada ya Ukraine kukamilisha ukarabati wa bomba lililoharibiwa kwenye mashambulizi. Umoja wa Ulaya unatarajiwa kutoa idhini ya mwisho kuhusu mkopo wa euro bilioni 90 kwa Ukraine.
- Iran yakataa kufungua Hormuz, mvutano na Marekani wazidi kuathiri uchumi wa dunia April 23, 2026Mvutano kati ya Iran na Marekani umeingia hatua mpya, huku Mlango Bahari wa Hormuz ukiwa kitovu cha mgogoro unaotikisa uchumi wa dunia. Licha ya kusitishwa kwa mashambulizi ya moja kwa moja, vita ya kiuchumi inaendelea.
- Iran yasema haitafungua tena Hormuz kama mzingiro wa Marekani utaendelea April 23, 2026Iran imeapa kutofungua tena Mlango-Bahari wa Hormuz kama mzingiro uliowekwa na jeshi la wanamaji la Marekani litaendelea kuwepo licha ya kuongezwa muda wa makubaliano ya kusitisha mapigano.
- Kane afunga tena wakati Bayern ikitinga fainali ya DFB Pokal April 23, 2026Bayern Munich imepiga hatua kuelekea kushinda mataji matatu, kwa kutinga fainali ya Kombe la Shirikisho la Ujerumani – DFB Pokal kwa mara ya kwanza tangu 2020. Bayern waliwafunga Bayer Leverkusen 2 – 0 Jumatano usiku.
- Vita Iran yachochea mzozo wa mafuta usafiri wa ndege Afrika April 22, 2026Vita vya Iran vinaongeza bei za mafuta ya ndege, hali inayozilazimisha kampuni za ndege barani Afrika kuongeza nauli, kufuta baadhi ya safari na kubadili mipango ya uendeshaji ili kuendelea kuwa na uwezo wa kifedha.
- Urusi yazuia mafuta ya Kazakhstan kwenda Ujerumani April 22, 2026Ujerumani imethibitisha kuwa Urusi itazuia mtiririko wa mafuta ya Kazakhstan kuelekea kiwanda muhimu cha kusafisha mafuta kinachochangia kwa kiasi kikubwa mahitaji ya nishati ya mji wa Berlin kuanzia Mei Mosi.
- IRGC yazuia meli mbili kwenye Mlango Bahari wa Hormuz April 22, 2026Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu la Iran IRGC limesema kikosi chake cha wanamaji kinazishikilia meli mbili zilizokuwa zikijaribu kuvuka Mlango Bahari wa Hormuz.
- Mabomu Hormuz: Ni tishio kiasi gani kwa usafiri baharini? April 22, 2026Hofu ya mabomu ya majini katika Mlango wa Hormuz yanaibua wasiwasi wa usalama wa meli, huku mataifa yakijadili hatua za kusafisha njia hiyo muhimu ya kimataifa inayopitisha asilimia 20 ya biashara ya mafuta na gesi.
- Papa Leo XIV atembelea gereza tata Guinea ya Ikweta April 22, 2026Ziara ya Papa Leo XIV katika gereza lenye utata nchini Guinea ya Ikweta yafufua mjadala wa haki za binadamu, mateso ya wafungwa na urejeshaji wa wahamiaji kutoka Marekani.
- Kahawa ilivyobadili maisha ya familia za wagonjwa wa celebral palsy Kenya April 22, 2026Kilimo cha kahawa nchini Kenya kinageuka kuwa tumaini jipya kwa familia za watoto wenye Cerebral Palsy, zikikabiliana na changamoto za malezi na kujitegemea kiuchumi.
