Swahili News
- Maafisa wawili wakuu wa CHADEMA waliokamatwa wameachiliwa April 25, 2025Chama kikuu cha upinzani nchini Tanzania CHADEMA kimesema viongozi wake wawili waliokamatwa na polisi wakiwa njiani kwenda mahakamani kuhudhuria kesi dhidi ya kiongozi wao wameachiliwa.
- Vurugu zashuhudiwa Vatican watu wakiendelea kumuaga Papa April 25, 2025Vurugu zimeshuhudiwa nje ya Vatican huku umati mkubwa wa watu ukiendelea kumiminika leo katika Kanisa Kuu la Mtakatifu Petero kutoa heshima za mwisho kwa kiongozi wa kanisa Katoliki duniani Papa Francis.
- Wanajeshi wa Pakistan na India washambuliana huko Kashmir April 25, 2025Wanajeshi wa Pakistan na India wamefyetuliana risasi usiku wa Alhamisi katika eneo linalozozaniwa la Kashmir. Umoja wa Mataifa umeyatolea wito mataifa hayo yenye silaha za nyuklia kujizuia na kutochochea mvutano zaidi.
- Kongo na Rwanda kutia saini makubaliano ya amani April 25, 2025Kongo na Rwanda, leo zinapanga kusaini makubaliano ya kukuza amani na maendeleo ya kiuchumi mjini Washington, kama sehemu ya msukumo wa kidiplomasisa wa kusitisha ghasia.
- Vikosi vya India na Pakistan vyashambuliana Kashmir April 25, 2025Vikosi vya Pakistan na India, vimekabiliana kwa risasi katika bonde la Kashmir . Haya yamesemwa na maafisa wa Pakistan wakati mvutano kati ya mataifa hayo mawili hasimu yenye uwezo mkubwa wa nyuklia ukiongezeka .
- UN: Kambi ya Zamzam nchini Sudan yakaribia kuwa tupu. April 25, 2025Shirika la Umoja wa Mataifa la misaada ya kiutu OCHA, limeonya kuwa kambi ya wakimbizi ya Zamzam katika eneo la magharibi mwa Sudan inakaribia kuwa tupu hii ikiwa chini ya muda wa wiki mbili baada ya RSF kuiteka.
- Uingereza: Tuko tayari kuisaidia Ukraine kupata amani April 25, 2025Waziri wa mazingira wa Uingereza Steve Reed, amesema wako tayari kuisaidia Ukraine kwa namna yoyote linapokuja suala la kuiunga mkono katika kutafuta makubaliano ya amani.
- Maelfu wanaendelea kumuaga Papa Francis leo April 25, 2025Maelfu ya watu wameendelea kujitokeza kutoa heshima zao za mwisho kwa aliyekuwa kiongozi wa Kanisa Katoliki duniani, Papa Francis katika Kanisa Kuu la Mtakatifu Petro mjini Vatican.
- Wapalestina huenda wakateua makamu wa rais kumsaidia Abbas aliyezeeka April 24, 2025Maafisa watiifu kwa Rais Mahmoud Abbas wanakutana kupiga kura juu ya kuanzishwa kwa nafasi ya makamu wa rais, na huenda wakamchagua mrithi mtarajiwa wa kiongozi huyo ambaye hana umaarufu na ana umri wa miaka 89.
- Mzozo wazidi kufukuta kati ya India na Pakistan baada ya shambulio Kashmir April 24, 2025Mvutano kati ya mataifa hasimu ya India na Pakistan umeongezeka kwa kasi, baada ya India kuilaumu Pakistan kwa shambulio la kutisha katika eneo la Kashmir siku ya Jumanne, na kuua watu 26, wengi wao wakiwa watalii.
- DR Kongo, M23 watoa ahadi ya pamoja kufikia mapatano April 24, 2025Serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo na kundi la waasi la M23 wametoa tamko la pamoja siku ya Jumatano, wakitangaza kuwa wamekubaliana kusitisha mapigano katika eneo la mashariki mwa nchi hiyo.
- Ukraine yasema haitatambua uhalali wa Urusi kuidhibiti rasi ya Crimea April 24, 2025Rais Volodymyr Zelensky wa Ukraine amesema Kyiv inaweza kufanya kila kitu ambacho washirika wake wanakitaka lakini haitatambua uhalali wa Urusi kuinyakua Crimea ambao ni kinyume cha sheria kulingana na katiba ya Ukraine.
- Kesi ya Lissu chini ya ulinzi mkali jijini Dar es Salaam April 24, 2025Ulinzi mkali wa Jeshi la Polisi umeimarishwa katika viunga vya mahakama ya mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam na maeneo mengine wakati kesi inayomkabili mwenyekiti wa Chadema Taifa Tundu Lissu ikisikilizwa.
- Maelfu kuendelea kutoa heshima ya mwisho kwa Papa Francis April 24, 2025Dunia inaendelea kuomboleza kifo cha kiongozi wa Kanisa Katoliki duniani Papa Francis, aliyeaga dunia Jumatatu wiki hii akiwa na umri wa miaka 88, baada ya kuugua kwa muda mrefu. Papa Francis atazikwa Jumamosi.
- Waandishi Habari wahatarisha maisha kuripoti mzozo wa Sudan April 23, 2025Mwaka mmoja tangu kuripuka kwa mapigano kati ya jeshi linaloitii serikali na kikosi cha wanamgambo wa RSF nchini Sudan, hali ya usalama kwa waandishi wa habari wanaoripoti mapigano hayo inazidi kuwa tete.