Swahili News
- Trump: Iran isalamu amri, hakuna mazungumzo March 6, 2026Rais Donald Trump wa Marekani amesema hakutakuwa na mazungumzo wala makubaliano na utawala wa sasa wa Iran na ameitaka nchi hiyo "isalimu amri" kama sharti kwa Washington kusitisha vita vinavyoendelea.
- Israel yazishambulia Iran na Lebanon, Tehran yajibu mapigo March 6, 2026Ndege za kivita za Israel zimeishambulia miji ya Beirut na Tehran leo huku kukiwa hakuna dalili ya kumalizika kwa vita vinavyoelekea kutimiza wiki nzima kesho Jumamosi.
- Wairani washiriki Ijumaa ya kwanza tangu kuanza kwa vita March 6, 2026Maelfu ya watu walijitokeza kwenye miji kadhaa nchini Iran leo kwa ibada ya kwanza ya Ijumaa tangu kuanza kwa vita baada ya Marekani na Israel kuishambulia kwa pamoja dola hiyo ya uajemi Jumamosi iliyopita.
- Mapigano yasababisha vifo vya watu 51 Sudan March 6, 2026Watu wapatao 51 wameuawa katika kipindi cha siku mbili zilizopita kufuatia mapigano yaliyozuka kusini wa jimbo la Kordofani nchini Sudan katika ya vikosi vya jeshi la taifa na wanamgambo wa RSF.
- Jeshi la Kongo lakamata silaha za kijeshi Ituri March 6, 2026Jeshi la Jamhuri ya Kidemorkasia ya Kongo (FARDC) limetangaza kukamata shehena kubwa ya silaha zilizofichwa kwenye eneo moja la mgodi katika jimbo la Ituri mashariki mwa nchi hiyo.
- Mgogoro Hungary na Ukraine ´wapamba moto´ March 6, 2026Hungary imesema itawafukuza raia 7 wa Ukraine iliowakamata wakisafiri na kiwango kikubwa cha fedha hatua ambayo serikali ya Ukraine imeiilaani.
- Mashambulizi kati ya Pakistan na Afghanistan yazidi kuibua mashaka March 6, 2026Pakistan na Afghanistan wameanza tena kushambuliana Ijumaa. Umoja wa Mataifa umesema mzozo huo baina ya mataifa hayo ulioendelea kwa karibu wiki moja sasa tayari umesababisha watu zaidi ya 100,000 kuyakimbia makazi yao.
- Halmashauri Kuu ya Umoja wa Ulaya yamkosoa Zelenskiy March 6, 2026Halmashauri Kuu ya Umoja wa Ulaya imemkosoa vikali Rais wa Ukraine Volodymyr Zelenskiy kwa kumtishia Waziri Mkuu Viktor Orban.
- Marekani yasifu operesheni yake nchini Iran March 6, 2026Marekani imesifu operesheni yake nchini Iran na kusema inaelekea kumuangamiza adui hata kabla ya wakati huku ikisisitiza kuwa uwezo wa mashambulizi wa Iran umepungua maradufu ukilinganisha na siku ya kwanza ya vita.
- Mapigano Kordofan kusini yawauwa watu 51 March 6, 2026Mapigano makali yanaendelea kushika kasi katika eneo la Kordofan kusini mwa Sudan, yakisababisha vifo vya makumi ya watu na kuzidisha mateso kwa raia.
- Rais wa Ujerumani aifuta ziara yake Indonesia March 6, 2026Rais wa Ujerumani Frank-Walter Steinmeier ameiahirisha ziara yake kuelekea Indonesia na Ufilipino kutokana na vita vya Marekani na Israel dhidi ya Iran.
- Mkataba wa Umoja wa Mataifa unaojadiliwa wakati migogoro inapotokea March 6, 2026Shambulio la Marekani na Israel dhidi ya Iran linaangaziwa kwenye Mkataba wa Umoja wa Mataifa. Kifungu cha 2(4) kinajitokeza wazi katika hali ya sasa. Ni kwa namna gani hasa?
- Marekani na Israel zaendelea kushambuliana na Iran March 6, 2026Israel imeendelea kuzishambulia Iran na Lebanon huku Marekani ikiishambulia pia meli ya kivita ya Tehran. Iran nayo imejibu kwa kuzishambulia nchi za ghuba huku milipuko kadhaa ikisikika pia mjini Tel Aviv.
- Israel yaishambulia Tehran, Iran 'yaitwanga' Tel Aviv March 6, 2026Hali inazidi kuwa tete katika eneo zima la Mashariki ya Kati huku Iran ikiendelea kujibu mashambulizi kwa kuilenga Israel na vituo vya kijeshi vya Marekani kwenye baadhi ya nchi washirika wa taifa hilo kubwa.
- Msalaba Mwekundu: Habari potofu adui mpya katika maeneo ya maafa March 5, 2026Shirika la Msalaba Mwekundu limeonya kuwa kuongezeka kwa taarifa potofu duniani kumeanza kudhoofisha juhudi za misaada ya kibinadamu na hivyo kuyatumbukiza maisha ya watu kwenye hatari.
