Swahili News
- Friedrich Merz aleta mtindo mpya wa siasa nchini Ujerumani June 8, 2025Ziara ya Kansela Friedrich Merz mjini Washington imepokelewa vyema nyumbani, huku wengi wakisifu mtindo mpya wa siasa unaotofautiana na ule wa watangulizi wake, Olaf Scholz na Angela Merkel.
- Israel yapanga kuizuia meli ya misaada ya kina Greta Thunberg kuingia Gaza June 8, 2025Israel imewaua Wapalestina wasiopungua 36, wakiwemo sita waliouawa karibu na kituo cha usambazaji wa misaada. Wakati huo huo, meli ya kibinadamu iliyombeba mwanaharakati Greta Thunberg iko njiani kuelekea Gaza.
- Ujerumani yacharazwa 2-0 na Ufaransa June 8, 2025Mechi ya mshindi wa tatu katika Kombe la Mataifa Ulaya ( UEFA NATIONS LEAGUE) kati ya wenyeji Ujerumani na Ufaransa imekamilika kwa wenyeji kulazwa 2-0.
- Wapalestina 10 wauawa Gaza wakati wakitafuta msaada wa chakula June 8, 2025Shirika la ulinzi wa raia wa Gaza limesema mashambulizi ya Israel leo Jumapili yamewaua takriban watu 10 wakiwemo wasichana wawili katika Ukanda huo.
- Trump atuma wanajeshi kuwadhibiti waandamanaji wahamiaji LA June 8, 2025Rais wa Marekani Donald Trump ameamuru wanajeshi wa kitengo maalum kutumwa mjini Los Angeles baada ya maandamano dhidi ya uvamizi wa wahamiaji.
- Urusi na Ukraine kubadilishana wafungwa wiki ijayo June 8, 2025Mamlaka nchini Ukraine imesema kwamba mpango wa kubadilishana wafungwa naUrusiutaanza wiki ijayo baada ya pande zote mbili kulaumiana kwa kujaribu kuzuia na kuchelewesha mabadilishano.
- Shambulio la Israel laua wanne Gaza June 8, 2025Maafisa wa Afya wa Palestina wamesema watu wanne wameuawa na wengine kadhaa kujeruhiwa na vikosi vya Israel katika eneo la karibu na kituo cha misaada kinachoendeshwa na shirika linaloungwa mkono na Marekani la GHF.
- Urusi na Ukraine zashambuliana usiku kucha June 8, 2025Urusi imefanya mashambulizi katika eneo la kati la Ukraine usiku wa kuamkia leo na kusababisha kifo cha mtu mmoja na kufanya uharibifu mkubwa wa mali, maafisa nchini humo wamesema.
- Kundi la Wagner kuondoka lakini Urusi itaendelea kuwepo Mali June 7, 2025Kundi la mamluki wa Urusi la Wagner limesema linaondoka kutoka Mali na kurejea nyumbani baada ya kusaidia kurejesha udhibiti wa serikali kwenye majimbo yote ya nchi hiyo
- Serikali ya Ethiopia yaidhinisha ongezeko la bajeti yake June 7, 2025Baraza la mawaziri nchini Ethiopia limeidhinisha bajeti ya takriban dola bilioni 15 za Kimarekani kwa mwaka wa fedha wa 2025/2026 unaoanza Julai, ikiwa ni ongezeko la asilimia 31 ikilinganishwa na mwaka uliopita.
- Mitihani yaendelea Kongo mashariki, licha ya usalama tete June 6, 2025Makumi kwa maelfu ya wanafunzi wa shule za sekondari mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo kunakoshikiliwa na waasi, wiki hii wamekalia mitihani ya kitaifa.
- Uhusiano wa Trump na Musk waingia dosari June 6, 2025Uhusiano wa karibu kati ya Rais wa Marekani Donald Trump na bilionea Elon Musk sasa umeyumba vibaya, baada ya mabishano yao makali kwenda hadharani kupitia mitandao ya kijamii.
- Mgogoro wa Cameroon ni miongoni mwa iliopuuzwa zaidi duniani June 6, 2025Baraza linaloshughulikia masuala ya wakimbizi la Norway NRC limetowa ripoti inayosema, Cameroon iko katika mgogoro mkubwa wa kibinadamu uliopuuzwa ambao umeipiku hali iliyokuwa ikishuhudiwa nchini Burkina Faso.
- Waislamu duniani kote waadhimisha Sikukuu ya Eid al-Adha June 6, 2025Katika mji mtakatifu wa Makka, zaidi ya mahujaji milioni 1.6 leo wamekuwa wakitekeleza ibada ya mwisho katika Hijja ya mwaka huu ambayo ni kumpiga mawe Shetani.
- Waislamu washerehekea sikukuu ya Eid Al-Adha June 6, 2025Leo ni sikukuu ya Eid-ul-Adh-haa inayoadhimishwa na Waislamu kote ulimwenguni kufuatia kukamilika kwa ibada ya Hijja kwa waumini wa dini hiyo, Makkah, nguzo mojawapo kati ya nguzo tano za Uislamu.