Swahili News
- Siku ya Wanawake wa Vijijini: Changamoto na mchango wa wanawake katika maendeleo October 15, 2024Dunia inaadhimisha siku ya wanawake waishio vijijini huku ikielezwa kuwa kundi hilo linakabiliwa na changamoto lukuki ikiwamo ukosefu wa elimu, ardhi, fursa za maendeleo, sambamba na kuathiriwa na mila kandamizi.
- Iran yalaani vikwazo vipya dhidi yake October 15, 2024Yanayoenedelea Mashariki ya Kati. Iran imelaani vikwazo vipya vilivyowekwa dhidi yake na Umoja wa Ulaya na Uingereza. Marekani yawasilisha mfumo wa ulinzi wa anga wa kisasa nchini Israel
- HRW: Rwanda inakiuka haki za binaadamu magerezani October 15, 2024Shirika la kimataifa la utetezi wa haki za binaadamu la Human Rights Watch limechapisha ripoti mpya inayosema, mamlaka nchini Rwanda zinafanya ukiukaji mkubwa wa haki za binaadamu magerezani, ikiwemo kuwatesa wafungwa.
- Idadi ya ndovu Kenya yafikia 36,280: KWS wahamisha ndovu 50 October 15, 2024Idadi ya ndovu nchini Kenya imeongezeka zaidi ya maradufu na kufikia 36,280. Hali hii imeilaazimu idara ya wanyamapori (KWS) kuwahamisha tembo 50 kutoka hifadhi ya kitaifa ya Mwea hadi Aberdares ili kupunguza msongamano.
- Mahakama Kenya yakataa kuzuia kura ya seneti kuhusu kumng'oa madarakani naibu wa rais October 15, 2024Mahakama Kuu nchini Kenya Jumanne ilikataa kuzuwia kura ya wiki katika Baraza la Seneti kuhusu iwapo kumuondoa mamlakani Naibu wa Rais Rigathi Gachagua. WIki iliyopita bunge la taifa lilipiga kura kumg'oa Gachagua.
- Upinzani Afrika Kusini wasema ni aibu kutomshitaki Ramaphosa October 15, 2024Kiongozi wa chama cha Umkhonto we Sizwe amesema hatua ya mkurugenzi wa mashtaka ya umma jimboni Limpopo kutomshtaki Rais Cyril Ramaphosa, katika sakata tata la ufisadi na utakatishaji fedha ni aibu kwa Afrika Kusini.
- Makubaliano ya matumizi ya maji katika Bonde la Mto Nile yaanza kutekelezwa October 15, 2024Ushirikiano wa kikanda wa nchi 10 umesema makubaliano kuhusu matumizi sawa ya rasilimali za maji katika Bonde la Mto Nile, yameanza kutekelezwa, licha ya upinzani kutoka Misri.
- ICC kuanzisha tena uchunguzi wa uhalifu Kongo October 15, 2024Mwendesha mashtaka wa ICC Karim Khan amesema ataanzisha upya uchunguzi wa madai ya uhalifu uliofanyika tangu mwaka 2022, katika jimbo linalokumbwa na migogoro mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.
- Mkutano wa kikanda kuanza Islamabad chini ya ulinzi mkali October 15, 2024Mkutano mkubwa wa kikanda unaanza leo kwenye mji mkuu wa Pakistan, Islamabad, chini ya ulinzi mkali.
- Taiwan: Ndege 153 za kijeshi za China zashiriki mazoezi ya kijeshi Taiwan October 15, 2024Wizara ya Ulinzi ya Taiwan imesema imegundua ndege 153 za kijeshi za China zinazoshiriki katika mazoezi ya kijeshi kwenye kisiwa hicho.
- Iran yalaani vikwazo vipya vya Umoja wa Ulaya dhidi yake October 15, 2024Iran imelaani vikwazo vipya vilivyowekwa na Umoja wa Ulaya na imekanusha kuipatia Urusi makombora.
- Mashambulizi ya Israel yawaua watu 40 Gaza October 15, 2024Mashambulizi ya jeshi la Israel yameuwa Wapalestina takribani 40 katika Ukanda wa Gaza.
- Mawaziri wa EU wagawika kuhusu mzozo wa Mashariki ya Kati October 14, 2024Mawaziri wa masuala ya kigeni wa Umoja wa Ulaya waliokutana Luxembourg, siku ya Jumatatu wameonesha mgawanyiko kuhusu mzozo wa Mashariki ya Kati unaoendelea kati ya Israel na makundi ya Hezbollah na Hamas.
- India, Canada zafukuziana mabalozi katikati mwa mzozo wa kidiplomasia October 14, 2024India na Canada zimeingia kwenye mgogoro mkubwa wa kidiplomasia baada ya kila moja kufukuza mabalozi na wanadiplomasia wa nchi nyingine, kufuatia mvutano juu ya mauaji ya kiongozi wa Masingasinga alietaka kujitenga.
- China yadhihirisha nguvu kubwa kwa kufanya mazoezi ya kivita karibu na Taiwan October 14, 2024China imefanya tena mazoezi ya anga na baharini karibu na Taiwan. Kisiwa hicho kinachojitawala kimelaani kitendo hiki "cha kichochezi." Taiwan pia imemkamata raia wa China kwa kuingia ardhi yake kinyume cha sheria.