Swahili News
- Merz awaalika viongozi wa Ulaya kabla ya mkutano wa NATO June 24, 2026Viongozi wa nchi tano zenye nguvu zaidi Ulaya wanakutana Jumatano mjini Berlin kwa mwaliko wa Kansela wa Ujerumani Friedrich Merz, ikiwa ni wiki mbili kabla ya mkutano wa kilele wa NATO uliopangwa kufanyika Uturuki.
- IAEA: Wakaguzi wetu kufika Iran hivi karibuni June 24, 2026Mkuu wa Shirika la Kimataifa la Nishati ya Atomiki (IAEA), Rafael Mariano Grossi, amesema wakaguzi wa shirika hilo wanatarajiwa kutembelea vituo vya Iran vya shughuli za kurutubisha madini ya urani hivi karibuni.
- Urusi yasema Ulaya haieleweki kuhusiana na vita Ukraine June 24, 2026Ikulu ya Kremlin leo imetilia mashaka utayari wa Ulaya kushiriki katika mazungumzo ya kumaliza vita nchini Ukraine na kurejesha uhusiano na Urusi.
- Rubio akutana na Rais wa UAE ziarani Mashariki ya Kati June 24, 2026Waziri wa mambo ya nje wa Marekani, Marco Rubio, amefanya leo mazungumzo na kiongozi wa Umoja wa Falme za Kiarabu Mohammed bin Zayed Al Nahyan wakati wa ziara yake Mashariki ya Kati.
- Ufaransa yatangaza kisa cha kwanza cha ugonjwa wa Ebola June 24, 2026Ufaransa imetangaza leo kisa chake cha kwanza kilichothibitishwa cha ugonjwa wa Ebola kugunduliwa ndani ya eneo lake, kinachomhusisha daktari aliyerejea kwa ndege kutoka Kongo.
- Senegal yapata pigo baada ya Edouard Mendy kupata jeraha June 24, 2026Timu ya taifa ya Senegal imepata pigo kuelekea mchezo wake wa mwisho wa Kundi I baada ya kuthibitishwa kuwa kipa wao tegemeo, Edouard Mendy, hatashiriki katika pambano la Ijumaa dhidi ya Iraq kufuatia jeraha la goti.
- Libya yapiga marufuku kuingia nchini humo raia wa nchi nne June 24, 2026Mamlaka za eneo la mashariki mwa Libya, zimepiga marufuku kuingia nchini humo kwa watu kutoka nchi nne jirani za Afrika. Hatua hii inaonekana kulenga kupunguza wimbi la wahamiaji wanaotaka kusafiri kuelekea Ulaya .
- Libya ya mashariki yazuia kuingia kwa raia wa Sudan, Somalia, Ethiopia na Eritrea June 24, 2026Mamlaka za mashariki mwa Libya zimepiga marufuku raia wa Sudan, Eritrea, Ethiopia na Somalia kuingia nchini, hatua inayolenga kudhibiti wimbi la wahamiaji wanaoelekea Ulaya kupitia Libya.
- Iran: Makubaliano ni ''tangazo la kushindwa kwa Marekani'' June 24, 2026Mkuu wa timu ya upatanishi ya Iran, Mohammad Bagher Qalibaf, amesema leo kuwa makubaliano yanayoendelea kati ya nchi yake na Marekani ni "tangazo la kushindwa la Marekani".
- DR Congo: Njaa yawasukuma wachimba dhahabu eneo la Ebola June 24, 2026Maelfu ya wananchi wanaotegemea uchimbaji wa dhahabu kwa maisha yao ya kila siku Kongo, wanakabiliwa na chaguo gumu kati ya kujikinga dhidi ya ebola au kutafuta riziki za familia zao.
- Iran: Makubaliano yanamaanisha kushindwa kwa Marekani June 24, 2026Iran inasema kilichothibitika hadi sasa ni kushindwa kwa ubabe wa Washington, huku Shirika la Nguvu za Atomiki Duniani (IAEA) likishikilia kupatiwa fursa ya kuendeleza ukaguzi kwenye vinu vya nyuklia vya Iran.
- Hatimaye Lungu kuzikwa Afrika Kusini June 24, 2026Mgogoro kuhusu mahali pa mazishi ya aliyekuwa Rais wa Zambia, Edgar Lungu, umefikia mwisho baada ya familia ya kiongozi huyo wa zamani kushinda kesi dhidi ya serikali ya Zambia katika mahakama ya rufani ya Afrika Kusini.
- Iran na Marekani zatofautiana kuhusu vipengele vya makubaliano ya kumaliza vita June 24, 2026Iran imekanusha kauli ya rais wa Marekani kwamba ilikubali ukaguzi wa nyuklia "usio na kikomo," ikisema haijafikia makubaliano yoyote ya aina hiyo wakati wa mazungumzo ya amani yaliyofanyika nchini Uswisi.
- Trump asema Iran imeruhusu wakaguzi wa nyuklia kuingia nchini humo June 23, 2026Rais wa Marekani Donald Trump amesema Iran imekubali kuwaruhusu wakaguzi wa nyuklia kurejea nchini humo, na kwamba vikosi vya jeshi la majini la Marekani havitouzuia tena Mlango Bahari wa Hormuz.
- Suala la Lissu na Polepole latua Bunge la Ulaya June 23, 2026Kamati ya Bunge la Ulaya kuhusu haki za binadamu imefanya kikao cha kusikiliza hali ya haki za binadamu nchini Tanzania.
